BENKI Kikuu Tanzania (BoT), imesema imeamua kuchukua usimamizi wa benki ya Twiga (Twiga Bancorp Limited), kuanzia Oktoba 28 mwaka huu.
Uamuzi huo umechukuliwa baada ya kubaini kuwa benki ya Twiga ina upungufu mkubwa wa mtaji kinyume na matakwaya sheria ya mabenki na taasisi za fedha ya mwaka 2006 na kanuni zake.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Gavana wa BoT, Prof. Beno Ndulu, alisema upungufu huo wa mtaji unahatarisha usalama wa sekta ya fedha na pia kuendelea kutoa huduma za benki kwa benki ya Twiga kuhatarisha usalama wa amana za Wateja wake.
Alisema kutokana na uamuzi huo, BoT, imesimamisha Bodi ya Wakurugenzi na uongozi wa benki ya Twiga na imemteua Meneja Msimamizi ambaye atakuwa na jukumu la kusimamia shughuli za Benki Kuu.
Prof. Ndulu, alisema pia umma unaarifiwa kuwa katika kipindi kinachokadiriwa kufikia wiki moja, kuanzia leo, shughuli za utoaji wa Huduma za kibenki za benki hiyo ya Twiga zitasimama ili kutoa nafasi kwa ajili ya kupanga taratibu za uendeshaji wa benki hiyo.
Alsema BoT, inauhakikishia umma kuwa itaendelea kulinda masilahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta ustahimilivu katika sekta ya fedha.

Advertisement

0 comments:

Post a Comment

 
Top