Jeshi la Polisi jijini Nairobi nchini Kenya linafanya uchunguzi kuweza kubaini kama mtu mmoja aliyeuawa jana karibu na ubalozi wa Marekani alikuwa amekula njama za kushirikiana na watu wengine kufanya shambulio.
Mtu huyo (24) aliuawa jana asubuhi nje ya ubalozi wa Marekani Nairobi baada ya kumshambulia mlinzi kwa kumchoma na kisu tumboni ndipo Afisa mwingine wa Polisi akampiga risasi kichwani.
Inadaiwa kuwa kijana huyo alikuwa akilazimisha kuingia ndani ya ubalozi huo, na mlinzi alipomzuia ndipo akamchoma kwa kisu.
0 comments:
Post a Comment