Na Ally Daud-Maelezo
Hayo yamesemwa naKatibuMkuuwaWizara
ya Ujenzi, Uchukuzi naMawasiliano Prof. FaustinKamuzora wakati wa kukabidhi matokeo
ya utekelezaji wa mradi kwa vijana wa mafunzo ya mambo ya Tehama na habari ambao
umejumuisha vijana kutoka sehemu mbalimbali nchini ambao umefanyika jijini Dar es
salaam.
“Vijana wanatakiwa wawe wabunifu
ili waweze kutumia fursa zilizopo kwenye Nyanja za uchumi wa Tehama kwa ujumla ili
waweze kunufaika na ubunifu wao kwa kujiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla”
alisema Prof. Kamuzora.
Aidha Prof. Kamuzora amesema
kuwa mradi huo ambao umefanyika kwa makubaliano ya Finland na Tanzania umegharimu kiasi cha
fedha za Euro milioni 6 utakamilika rasmi ifikapo Desemba mwaka huu ili kuweza kutoa
fursa kwa vijana kuchangia uchumi wa nchi katika sekta ya mawasiliano.
Kwa upande wake Mkurugenzi
wa Huduma za Mawasiliano wa Wizara hiyo Bi. Clarence Ichwekeleza alisema mradi huo
umelenga kuwapa vijana mafunzo ya jamii habari
ili kusaidia taifa kufikia katika uchumi maarifa ambao utatokana na maendeleo
ya Tehama.
“Watanzania hususani vijana
wanatakiwa kupata ujuzi wa Tehama na kuwa na uwezo wa Jamii Habari ili kuweza kuendelea
kiuchumi kwa kupitia maendeleo ya mawasiliano ili kuweza kuwa na uchumi maarifa
ambao ndio unaofanyika duniani kote hasa kwa nchi zilizoendelea” alisema Bi. Ichwekeleza.
Mradi huo ambao umewalenga
vijana kutoka katika sekta ya Tehama
umefanyika kwa ushirikiano kati ya
Tanzania na Finland umeanza mwaka 2011 na kutarajiwa kufikia tamati kwa kukamilisha
malengo yake Desemba mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment